Thursday, November 25, 2010

karibuni makaadi waugwana kwa idadi.


Na Hafidh Kido

Mwandishi Hafidh Athumani kido, ni mswahili aliezaliwa uswahilini na mwingi wa kufurahia ladha ya lugha adhimu ya kiswahili. Blogu hii ni ya kiswahili na mwandishi hufikiri namna dunia inavyokwenda. 

Kila uchao kuna mambo mapya yanayobangua vichwa vya wanaadamu. Ni fedheha sana kwa muungwana kushindwa kuidhibiti mihemko yake. Jina la ukurasa huu limeitwa 'picha na maneno,' kwa maana lugha zote duniani zinawakilishwa na vitu viwili, picha na maneno.

Mara zote tumekuwa ni watu wa kushindwa na mabadiliko ya kilimwegu. Mambo mengi hutokea kwa lengo la kututahini; lakini ni kweli kuwa tumeamua kuishi maisha ya walioshindwa? Jibu ni hapana, kwa kila mwenye kufikiri.

Najua sijapata wasaa wa kukukaribisha rasmi katika blogu hii yenye kuisadifu dunia na mambo yake, blogu yenye ladha ya Kiswahili kitamu kikwanguacho ndimi zetu laini. Karibu tafadhali ufaidi uhondo huu. 

Andamana nami katika ukurasa huu ili uweze kupata mafafanuzi ya mambo kadha yanayoonekana kutushinda kuyapatia maamuzi, aidha kwa uchache wa elimu ya dunia au uvivu wa kufikiri. Ahsante mswahili mwenzangu. 

Karibu ukaribie, ulo nayo unambie
Hofu tusizikimbie, nyufa tuzizibie
Kaburi tuwachimbie, waoga kina babie
Hekima jengo la busara, tuandamane nayo kwanza

No comments:

Post a Comment