Wednesday, October 20, 2010


KICHEFUCHEFU CHA HABARI KIMEANZA TANZANIA

Na Hafidh Kido

Mwaka jana nilihudhuria mdahalo wa wazi ulioandaliwa na jukwaa la majadiliano ya wanafunzi wa chuo chetu- Kampala International University (KIU Student Forum Debate), mdahalo ulihusu mswada wa uchaguzi kwa nchi za jumuia ya Afrika ya Mashariki.

“Will the proposed East African Election Bill solve the election problems in east African?” tafsiri yake “Je pendekezo la mswada wa uchaguzi kwa Afrika ya mashariki utatatua matatizo ya uchaguzi kwa nchi wanachama?” hicho ndicho kilikuwa kichwa cha habari cha mdahalo huo.

Mwanzoni mwa mwaka jana baadhi ya viongozi na wasomi kutoka nchi wanachama wa jumuia ya Afrika mashariki, walikutana jijini Kampala nchini Uganda, kujadili mswada wa uchaguzi wa pamoja kwa nchi wanachama ili kuepusha vurugu za uchaguzi, wakichukua hadhari kwa yaliyotokea Kenya mwaka 2005.

Walialikwa baadhi ya wabunge toka bunge la vijana wa Uganda, wengi walichangia kwa majibizano kama ilivyo hulka ya wabunge wetu hasa wakiwa wanatoka vyama tofauti. Lakini nilichokuja kugundua ni kuwa wote waliishia kutoa sababu zilizofanana ingawa waliamini wanatofautiana mawazo.

Mzungumzaji wa kwanza aliitwa bwana Asiimwe steven, kutoka chama tawala cha NRM (National Resistance Movement) cha bwana Museveni, Rais wa Uganda. Bwana Asiimwe, alisema kuwa ifike wakati vyama vya upinzani vikubaliane na ukweli hasa wa matokeo ili kuepusha vurugu za baada ya uchaguzi.

Alitoa kichekesho na kusema, “ ikiwa wapinzani wanadai Rais Museveni amezeeka basi na wao walete mtu mwenye sifa kama za Museveni, na si kulaumulaumu tu” alikwenda mbali zaidi pale alipowaambia wakenya “Wakenya msiwe na sifa juu ya Obama, tengenezeni Obama wenu, yule hawezi kuwa rais wa Kenya.”

Utaona maneno yake ni ya msingi kwa namna fulani, bwana huyu ingawa alimsifia kiongozi wake wa chama Generali Museveni, lakini utaona anahubiri amani. Haamini katika vurugu, ikiwa unadhani Museveni amezeeka basi mchague ‘Dk. Kizza Besiggye’ huyu ni kiongozi wa chama cha upinzani cha FDC (Forum for Democratic Change), na si kupiga kelele.

Mzunguzaji wa pili bwana Erick Sakwa, kutoka chama cha UPC (   ). Yeye anaamini katika utoaji wa taarifa sahihi. Anasema kuwa “taarifa ndiyo oxsijeni (oxygen) ya demokrasia. Hatuwezi kuanzisha jukwaa la kujadili mswada wa uchaguzi wa pamoja kwa nchi tano zenye historia tofauti za kisiasa bila ya kuzingatia viongozi wao wameingia madarakani kwa namna zipi”

Utaona hoja yake ipo kihistoria zaidi, ufinywaji wa taarifa juu ya historia za viongozi na vyama vyao ni suala la kuzingatia sana. Na hapa ndipo ninapopatia ufunguo wa mada ya makala haya. Hakika kichefuchefu kimeshaanza Tanzania, historia za viongozi wetu wanavyoingia madarakani tunajua wenyewe. Wizi, ulaghai na lawalawa kwa wananchi hushamiri katika kipindi cha uchaguzi.

Nipo mbali na nyumbani lakini si haba wa taarifa za kila linalojiri huko, nasikia viongozi wetu wameoa wake watatu- siasa, dini na taaluma ya uandishi wa habari. Kitakachofuata ni kuzaa watoto wenye mtindio wa ubongo. Maana watoto watakuwa wa baba mmoja ila hawapatani, ya Rwanda, Kenya, Burundi na Uganda kidogokidogo sasa yatahamia Tanzania.

Waswahili wana usemi wao kuwa mtu akiwa na tabia nzuri tangu utotoni na kuharibikiwa ukubwani huyo hufananishwa na mung’unya. Hivyo Tanzania yetu kisiwa cha amani imegeuka mung’unya kuharibikia ukubwani.

Katika mjadala ule kila nchi ilitoa sababu zake ni kwanini mswada huo wa uchaguzi wa pamoja hautoweza kutatua matatizo ya uchaguzi katika nchi tano hizi.

Wakenya walizungumzia  ukabila kuwa ndiyo sumu, maana kila kabila linataka mtu wao ndie aongoze nchi, na wakikuyu bado wanataka kuitawala Kenya- ukiangalia tangu baba wa taifa la Kenya Mzee Kenyatta, Moi na Kibaki, wote ni wakikuyu, hivyo hawataki kuiachia hiyo kamba.

Waganda wao walizungumzia ukabila na ujeshijeshi uliotawala Uganda. Maana Uganda mpaka sasa inatawaliwa kijeshi tangu mapinduzi ya mwaka 1986, yaliyomng’oa madarakani Tito Okello, nae alimtoa Milton Obote, mwaka 1985, Obote aliingia kwa uchaguzi mwaka 1980, ambapo kabla ya hapo alikuwapo Paulo Muwanya, aliekuwa mwenyekiti wa tume ya kijeshi iliyomtoa madarakani Godfrey Binaisa, 1979.

Binaisa yeye alimng’oa Yusuf Lule, aliewekwa na Mwalimu Nyerere baada ya kuondolewa Nduli Idi Amin Dada, mwaka 1979. Nae Idi Amin, alimtoa madarakani kijeshi Milton Obote, mwaka 1971, na Obote nae akisaidiwa na Idi Amin walimtoa Kabaka Muteesa, ambae alipokea uhuru mwaka 1962 kutoka kwa waingereza akisaidiwa na Benedicto Kiwanuka, ambae alishinda uchaguzi wa March 1,1961, chini ya chama cha Democratic Party (DP), na kuwa waziri mkuu wa kwanza wa Uganda huru.

 Lakini baadae walipoamua kuunganisha vyama vya DP cha Benedicto Kiwanuka na UPC cha Milton Obote, ndipo Obote akawa waziri mkuu wa pili chini ya Kabaka Muteesa, kama rais na mfalme wa Buganda Kingdom.

Utaona tangu Uganda ipate uhuru hali haikuwa nzuri, Museveni ndie rais wa kwanza kukaa madarakani kwa muda mrefu.

Kingine kinachoitafuna nchi ya Uganda ni ukabila, mpaka sasa Buganda Kingdom wanadai madaraka yao waliyonyang’anywa na Obote kutoka kwa Kabaka Muteesa, ambae alikuwa mfalme wa Buganda Kingdom na rais wa kwanza wa Uganda huru. Na mpaka sasa Buganda Kingdom wanataka Federal Government (Serikali ya majimbo) kama ilivyo Marekani.

Uganda kila kabila linaongozwa na mfalme, ina maana Museven ni kama anaongoza Serikali kuu akiwa Kampala tu, lakini kila kabila lina kiongozi wake wanawaheshimu kuliko rais wa nchi.

Na hapo palipo na Ikulu Kampala, ni eneo la Buganda Kingdom, serikali inatakiwa ilipe kodi kwa Buganda Kingdom, yaani kuna fungu linaingia kila mwaka katika serikali ya Buganda Kingdom na wana bunge lao linaitwa Lukiiko na wana waziri mkuu wao anaitwa Katikkiro kwa cheo, na jina lake ni J.B.Walusimbi. Mfalme wao wa sasa anaitwa Kabaka kicheo, jina lake halisi ni Ronald Mutebi, inakanganya eeenh!.

Mwaka jana jijini Kampala kulikuwa na vurugu baina ya Buganda Kingdom na Museveni, Kabaka Mutebi alikuwa anataka kuwatembelea watu wake sehemu fulani, lakini Museveni akataka kuonyesha yeye ni zaidi akamkatalia, kilichotokea ni wabaganda kulala barabarani, wakatumwa askari pamoja na wanajeshi kuwatawanya, ila kilichofuata ni mapigano, vita hasa.

Sisi hatukutoka kuenda mjini wala sokoni ni ndani tu, watu waliuwawa, wengine walipoteza viungo, redio za Buganda kingdom zilifungwa na baadhi ya wabaganda mpaka sasa wapo rumande wanasubiri kusomewa mashtaka.

Tanzania kukitokea vurugu huletwa FFU, lakini Uganda wanaletwa wanajeshi na vifaru, mabomu na kila silaha nzitonzito, ukiwanyooshea kidole tu umeumia.

Burundi na Rwanda hakukuwa na wachangiaji, lakini tunafahamu ingawa hali kwa sasa imetulia lakini ukabila na ujeshijeshi bado kuisha katika nchi hizo.

Tanzania mimi ndie nilechangia mada, lakini kabla sijasimama wachangiaji walionitangulia waliisifia nchi yetu kwa amani na utulivu. Wakasema Tanzania hakuna vurugu za baada ya uchaguzi, na nchi yetu ina amani na utulivu kiasi wao wanapaswa kuiga kwetu. Nilichekea kiganjani.

Sikutaka kuharibu jina la nchi yetu, lakini yaliyo moyoni Mungu mwenyewe ndie anaejua, maana huwa tunalazimishwa kujiua wenyewe, amani aliyoiacha Mwalimu Nyerere imeshapotea, siku hizi sauti za mabomu, milio ya risasi tumeshavizoea. Lakini hayo yote wenzetu hawayajui.

Nilichofanya ni kuwazindua kuwa ni kweli vurugu hakuna maana viongozi wetu wameshajua pa kutukamatia siku hizi, ni pahali padogo sana, ni kiasi cha kudhibiti imani mbili, ya dunia na akhera.

Imani ya dunia ni kudhibiti waandishi wa habari, ima kwa kuwatisha au kuwanunua, na imani ya akhera ni kuwadanganya waumini wa dini mbili kuu, uislamu na ukristo. Nakumbuka wakati Rais Kikwete anaomba kura mwaka 2005, aliitwa chaguo la Mungu na viongozi wa kikatoliki, na akapewa biblia ili imlinde.

Hakuishia hapo, akawaahidi waislamu kuwa atawaletea Kadhi ili aweze kutatua matatizo yao madogomadogo, lakini mpaka sasa ni wimbo. Hivyo mada yangu kuu ilikuwa ni kuwazindua wana Afrika mashariki wenzangu kuwa si kuwa Tanzania kuna amani ila tumetiwa mtungini sauti zetu hazitoki. Na uoga unatunyima kutukutika.

Hivyo naomba niseme kuwa kwa kuwa uchaguzi umebakia siku chache utaona ziara za viongozi wote lazima zitabeba waandishi wa habari. Bahasha zitakuwa nyingi na ziara za kutembelea vyombo vya habari hazitokwisha. Misikiti itapata mabusati mapya na kupakwa rangi, makanisa yatapata wageni rasmi wengi katika harambee za ujenzi wa majengo ya kanisa.

Harufu mbaya imeshaanza kusikika, kichefuchefu kitatusababishia kutapikia viatu vya wajumbe wa usimamizi wa zoezi la upigaji kura. Watakimbia kutoa taarifa za uongo, kumbe wanaepuka harufu ya matapishi. Naomba kuwasilisha.





woga ndicho kisababishi cha kuonewa katika jamii


Tujijue tuna michango gani ktk jamii tusiishi tu


Na Hafidh Kido

Katika maisha ni jambo jema sana kujijua unasimamia nini, ni ubaghili wa urithi kwa kizazi kijacho kusema mimi siamini kitu na wala sina upande wowote ninaosimamia. Ni vema kueleza msimamo wako kwa njia moja ya nyingi zilizotumiwa na wapigania haki.
Rais wa kwanza wa India Mahatma Gandhi, ni mmoja ya viongozi wanoheshimika sana duniani, alianzisha utaratibu wa kudai haki bila vurugu. Kwa kikoloni iliitwa ‘non violence agitation’ au mwenyewe kwa kihindi aliita {ganda satraha}, utaona ni namna Fulani hivi ya kiyonge ya kudai haki lakini imeleta mvuto na mwamko mkubwa katika dunia mpaka mpigania haki za weusi nchini Marekani Martin Luther King Jr nae aliiga mfumo huo wa kudai haki pasi na vurugu.
Lengo la kusema haya ni kutaka kuieleza dunia kuwa kudai haki ni haki ya kila mwanaadamu anaechukizwa na mfumo Fulani wa kiutawala au namna yoyote ya maisha isiyompendezea.
Lakini cha ajabu wapo watu ambao hubaki mfu huku wakiugulia moyoni, wato namna hiyo hata Mungu huwadharau. Ndiyo! hata Mungu huchukizwa na mtu anaedhulumiwa na asipaze sauti kudai haki yake. Ni ujinga ulioje kunyamazia upuuzi wa mtu mmoja aikoseaje jamii ya watu wapatao maelfu mengi, ni udhalili ulioje kujikunyata kwa hofu kwa kitu kikuyimacho uhuru wa kuabudu, kuamini au kuishi kwa amani kwa maisha uyalipiayo gharama kubwa. Hilo halivumiliki.
Jamii za kiafrika ziliishi katika unyonge kwa karne nyingi zilizokuwa chini ya ukoloni. Walitumishwa na kufanyishwa kazi ngumu ambazo hata hao waliowatumisha wasingeweza kufanya hata robo yake. Mababu zetu walijenga reli kwa kubeba vyuma vya reli katika migongo yao; jaribu leo hii kuyanyua chuma kimoja cha reli na ukibebe japo mita mia moja tu. Lakini chuma hicho hicho kilibebwa na mababu zetu kwa maili elfu bila ya kuchoka huku wakichapwa bakora. Na kila alieonyesha udhaifu aliuwawa kikatili. Udhalili ulioje huu.
Kina Mkwawa wa Uhehe walipojitokeza kudai haki za waafrika wenzao walitokea waafrika wasio na fikra na kuiba siri za viongozi wa kiafrika na kuzipeleka kwa wakoloni ili wapate ngawira kidogo ambazo hazikuwafaa chochote. Haiingii akilini kamwe.
Hata wakati wa kudai uhuru kina Kwame Nkurumah. Nyerere, Kenyata na wengi wengineo kama Robert Mugabe na Nelson Mandela walipata upinzani mkali kutoka kwa waafrika wenzao ambao walikuwa na nyoyo za woga. Ni dhuluma ya nafsi yako kuogopa kuomba haki.
Munaweza kupanga kugomea kuingia darasani ili chuo, shule au taasisi yoyote ipewa haki, lakini unakuta wapo wenzenu ambao wataendele kuingia darasani au kuenda kazini kama kawaida mradi tu wanaogopa kudai haki zao. Hakika inaudhi.
Mara nyingi watu namna hiyo husimamia ukweli kuwa hawataki fujo, lakini kidhati unapopingana na wenzako inaonyesha ni kiasi gani hujui kusimamia unachoamini. Unadhani kizazi kijacho kitanufaika vipi ikiwa wewe uliishi katika unyonge? Unadhani mwanao atanufaika vipi na utu bora ikiwa wewe uliishi katika kupinga mabadiliko? Unadhani mjukuu wako atajinasibisha vipi na wewe ikiwa muda wako wote wa maisha uliutumia katika hofu na kujificha? Unadhani baada ya miaka mia moja utaendelea kutajika ikiwa tu katika uhai wako hukuacha chachu yoyote au alama yoyote ya mabadiliko kwa hiyo miaka mia moja ijayo? Sidhani mtu muoga anayo majibu muafaka kwa maswali hayo. Hakuna  halitokuwapo.
Tunaishi katika dunia ya mashindano, kila mmoja anataka kuvutia upande wake kama muwamba ngoma. Lakini kikubwa ni kujitambua upo kundi gani ili uepukane na matatizo. Maana hatua ya kwanza ya kuepuka tabu ni kukubaliana na hali halisi.
Dunia ina watu wenye kujua mambo lakini wenyewe hawajui, hujiona ni watu wa kawaida sana lakini kauli zao hufuatwa na wanajamii kama nyuki afuatavyo maua.
Cha kushangaza watu namna hiyo hutumia vipawa vyao kuwaogofya watu na kuwakatisha tamaa. La busara ni kuwaamsha watu hao ili wafanye kitu wakijuacho kwa manufaa ya wengi.
Lakini kuna watu ambao hawajui na hawajui kuwa hawajui, ila tatizo lake ni kuwa wabishi wa kuonyeshwa njia. Huamini kila wakisikiacho na ni wakaidi wa kufuata waambiwacho. Mmmhhhh…. Watu namna hiyo ni bomu linalosubiri kulipuka, hutumia nusu ya maisha yao kuamini kisicho kweli. Ni vema kuwaepuka watu namna hiyo ili kusaidia wenye haja. Wadigo wana methali yao isemayo ‘mwana hukanywa akiuya’ maana yake mtoto mkaidi huambiwa ajirekebishe pale anapokubali kuwa alichofanya si sahihi na limeshampata la kumpata.
Kadhalika jamii imejaa watu wasiojua chochote katika maisha, lakini ni wepesi kuuliza kila wanaposhindwa kuelewa. Hao ni waja wema ambao wamesifiwa mpaka na Muumba mbingu na ardhi. Ni vema kuwaonyesha njia na kuwaelimisha, watu hao huwa waongofu kila waonapo ukweli na ni wepesi kuelimisha wenzao kila inapohitajika.
Jamii vilevile imezungukwa na watu wajuvi na wanajua kuwa wao ni wajuvi wa mambo kadha yasumbuayo watu katika jamii wanazoishi. Ni vema kuwa wafuasi wa watu namna hiyo. Wana mambo mengi ya kuturithisha kwa faida ya kizazi kijacho. Kuwaepuka ni sawa na kujaribu kuziba jua kwa kutumia sepetu, bila kudhani kuwa miale ya jua hupenya kila penye nukta ya upenyo.
Kifupi nilichotaka kuieleza jamii ni kusimamia haki zetu, tusiwe waoga kwa kusimamia ukweli. Kuwa msaliti wa nafsi yako ni kosa kubwa sana litakaloisababishia dunia kuangamia. Watu waoga ndiwo wasababishao mambo kuenda mrama, vita, taabu na maonevu huletwa kwa kuwa dunia inashikiliwa na watu waoga.
Acha uoga simamia haki yako, kuna manufaa makubwa kwa kizazi kijacho.

unaupingaje ufisadi kuanzia ngazi ya familia?


 JE? UFISADI NI IMANI KAMA ULIVYO UJAMAA

Na Hafidh Kido

Hayati mwalimu Nyerere katika maandiko yake yahusuyo ujamaa alipata kusema kuwa “ujamaa wa kweli ni mawazo ya mtu.” Akimaanisha kuwa ujamaa si kufuata sera yake au kumuonyesha mtu kuwa mimi ni mjamaa kamili, bali ni namna mtu anavyoamini na kuishi kijamaa.

Mwalimu alifafanua kuwa, “Ujamaa, kama demokrasia, ni moyoni. Katika nchi ya ujamaa kama unataka kuhakikisha kwamba watu wanajali shida za watu wengine, linalotakiwa ni mawazo ya kijamaa, wala siyo kufuatisha tu utaratibu maalum wa siasa.”

Na tunafahamu kuwa Mwalimu aliupiga vita ubepari ikiwemo rushwa kwa maisha yake yote, tangu akiwa shule, wakati wa mapambano ya kuleta uhuru, kipindi chake cha uongozi kama rais wa nchi na mwenyekiti wa chama tawala na hata alipostaafu.

 Machi 13, 1995, Mwalimu alipokuwa anazungumza na klabu ya waandishi wa habari wa Tanzania, katika hoteli ya Kilimanjaro, alipata kusema haya,“usije ukadhani kwamba wakati wa awamu ya kwanza palikuwa hapana rushwa; ilikuwapo, lakini tulikuwa wakali sana….. tulitaka watu wajue hivyo. Tulitaka watu wajue kwamba tutakuwa wakali sana na wala rushwa ndani ya serikali na wale wanaotoa rushwa.” Na hakika Mwalimu hakutania wala hakumuonea mtu haya. Aliwadhibiti wala rushwa kwa uwezo wake wote.

Yanayotokea sasa yanaweza kuzuilika ikiwa tu watanzania watamuenzi baba wa Taifa kwa vitendo, tofauti na kumuenzi kwa kunywa na kula siku ya kumbukumbu ya kifo chake. Wakati wa Mwalimu ufisadi uliweza kuzuilika kwa namna mbili.

Moja ni kwa kumdhibiti mtu anaetaka kuwa kiongozi, kwa maana aliwaandaa viongozi kuwa watumishi bora kwa wananchi. “Zamani, katika CCM na katika TANU, tunapochagua mgombea wetu, kama ana mali, tunamwambia ‘hii mali umeipata wapi?’ mali kilikuwa kigezo cha kukupotezea sifa ya kuwa mgombea.”

Jambo la pili Mwalimu alilolitumia kupiga vita rushwa kwa viongozi ni kutowaonea haya viongozi wa ngazi yoyote. Utaona kwamba mara tu baada ya kupata uhuru, waziri wa sheria wa Tanganyika alibainika kupokea rushwa, lakini Mwalimu aliacha sheria ichukue mkondo wake, hakutaka kufunikafunika wala kumung’unya maneno; alimuadhibu kama sheria ilivyotaka. Kwa kiasi utaona viongozi wote waliokuwa kipindi cha Mwalimu, kama bado wapo hai basi hawana mali nyingi kupita kiasi. Maana yake hawakula rushwa wala kujilimbikizia mali kama ilivyo sasa. 

Tunafahamu kuwa ufisadi ni ubepari uliokomaa, tena zaidi ya ubeberu. Lazima tujiulize kwa umakini kuwa huu ufisadi nao ni imani kama ulivyo ujamaa?

Sababu za msingi za kuuliza swali hili ni kutokana na kujirudiarudia kwa matukio ya kifisadi mbali ya viongozi wa dini, vyama vya siasa na vyombo vya habari kupiga kelele kila siku juu ya kukithiri kwa vitendo vya kifisadi. Lakini badala yake ndiyo vinaongezeka maradufu.

Msomi maarufu nchini na Profesa wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere, Chuo kikuu cha Dar es salaam, Profesa issa Shivji, alipokuwa akiwasilisha mada inayohusu mtazamo wa Mwalimu Nyerere juu ya ujamaa, ubepari na ufisadi; katika kongamano la kumbukumbu ya miaka kumi tangu kufariki Baba wa Taifa, ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee, Oktoba 12, 2009, alikuwa na haya ya kusema.

“Kwa vyovyote vile, Mwalimu hakuamini, wala sikumbuki kwamba alisema waziwazi kwamba anaamini kwamba ubepari ni imani. Ubepari ni mfumo, si imani,” alisisitiza.

Profesa Shivji aliongeza kuwa “Ulimbikizaji mtaji ndio kiini cha mfumo wa kibepari. Uhai wa bepari kama bepari hutegemea ulimbikizaji. Bila ulimbikizaji bepari hawezi kuishi kama bepari.”

Alipokuwa akilizungumzia suala la ufisadi alisema kuwa enzi za Mwalimu ufisadi haukuwapo, ila rushwa ilikuwapo. Mwalimu mwenyewe alikuwa akirudiarudia kauli hii ‘Rushwa ni adui wa haki,’ lakini msamiati wa ufisadi haukuwa katika serikali yake.

Hii ikimaanisha kuwa ufisadi ni rushwa iliyoota mizizi na kukua kuliko kawaida. Kwa mujibu wa Mwalimu rushwa ni kishawishi unachotoa ili mpokeaji aipinde sheria au taratibu rasmi kwa kumrahisishia mambo yake mtoaji.

Kwa mfano mtu anapotoa Kitu au fedha ili mgonjwa wake asikae katika foleni ya kumuona mganga, hiyo ni rushwa, na mpokeaji ataitumia kwa matumizi yake ya lazima au ya binafsi. Kwa maana nyingine pesa hiyo itatumika kulipia kodi na itarudi kwenye mzunguko. Kutakuwa na uvunjifu wa haki na utovu wa maadili, ila uchumi wa  nchi hauwezi kuyumba kwa rushwa hiyo.

Ufisadi ni neno la Kiswahili linalotokana na lugha ya kiarabu lenye maana ya kuharibu au uharibifu. Mtu anapoitwa fisadi maana yake ni muharibifu wa jambo au kitu. Hivyo mafisadi ni waharibifu wa mali za umma na uchumi kwa ujumla. Ni wa kuogopwa.

Profesa Shivji anaamini kuwa mfumo wa uliberali mamboleo ndiwo uliozaa ufisadi. Labda utajiuliza uliberali mambo leo ndiyo nini?

Kutokana na makala yaliyochapishwa na gazeti la wiki la Raia Mwema, ukurasa wa 19, toleo namba 112 la tarehe 16 Desemba, 2009.  Profesa Shivji anaeleza kuwa: Misingi mikuu ya mfumo wa uliberali mamboleo ni:
. Ulegezaji wa masharti ya biashara ya nje na ndani, kwa maana ya kwamba serikali haidhibiti tena biashara.
. Ulegezaji wa masharti ya soko la fedha na fedha kwa ujumla, kwa maana kwamba yeyote yule anaweza akaingiza na kutoa fedha nchini bila kudhibitiwa. Kwa kifupi, kuwa na soko huria katika bidhaa na fedha.

Hayo ni masharti ya wafadhili na taasisi za kibeberu. Maana yake ni kuwa serikali inapoteza uwezo na haki yake ya kujiamulia mambo muhimu ya sera na mwelekeo wa nchi kwa faida ya watu wake kinyume na ilivyoainishwa katika katiba yetu  kuwa, “watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya mamlaka ya Nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhirifu, na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao”.

Katika kijitabu cha Azimio la Arusha, cha mwaka 1967 ukurasa wa 16, suala la uwekezaji linazungumziwa na Mwalimu Nyerere, kama moja ya njia za kujipatia fedha za nje, ila akasisitiza kuwa ni njia ya hatari. “Aina ya tatu, ambayo pia ni kubwa…. Ni ile ya fedha za watu au makampuni yanayotaka kuja katika nchi yetu kuanzisha shughuli mbalimbali za uchumi kwa manufaa yao wenyewe. Na sharti kubwa walitakalo jamaa hawa wenye fedha zao ni kwamba shughuli yenyewe iwe ni ya faida kwao na pia kwamba serikali iwaruhusu kuondoa faida hiyo Tanzania na kuipeleka kwao. Hupenda pia kwa jumla serikali iwe na siasa wanayokubaliana nayo au ambayo haihatarishi uchumi wao.”

Utaona kwamba hali tuliyonayo sasa ya kukithiri kwa ufisadi ni kukomaa kwa kuzoeana katika mfumo wa kiuongozi. Urafiki na kuoneana haya ndivyo vilivyozaa ufisadi.

Swali langu la msingi linarudi palepale, ufisadi nao ni imani kama ulivyo ujamaa? Maana tangu kuasisiwa kwa ujamaa miaka ya sitini mpaka sasa wapo wazee ambao huwaambii kitu kuhusu imani yao juu ya ujamaa. Ukitaka kumuudhi mzee yeyote muasisi wa TANU, basi jaribu kumwambia ujamaa haufai, anaweza hata kukuchapa bakora japo hajimudu hata kuamka.

Hali inavyobashiri miaka kumi na zaidi ijayo ufisadi nao unaweza kuwa ni imani itakayobaki vichwani mwa wazee wa baadae, na kuamini kuwa ‘kula nchi’ ndiyo malipo ya usumbufu walioupata ima kwa kugombea nafasi fulani ya uongozi au kutafuta elimu.

Maana sasa ni wazi kuwa hata wanafunzi wa vyuoni wanauzungumzia ufisadi kwa mkabala wa ushujaa. Si ajabu kumkuta mwanafunzi wa shahada ya uhasibu akikuambia, “yaani elimu ninavyoipata kwa taabu hivi halafu nisiwe fisadi? Hiyo haiwezekani” jamani hii si ni hatari?
                                                



Tuesday, October 19, 2010

si fisadi alipata ajali ya kisiasa tu.

hapa nilikutana na rais wangu wa zamani wa chuo Kampala International University cha uganda, sasa ni dean of students KIU tawi la Dar es salaam, anaitwa Allute .

Sasa sijui nani anamuomba mwenzie. Kikwete anataka Kura mtoto anataka kula.

wapo waliosugua vichwa kwa ajili yetu. hivyo tusiharibu amani katika uchaguzi.

Fake smile

They fed us ever since we were not able to eat...

 









WHY SON NEED A MOM

1.       Who laughs at his jokes
2.       Who will indulge his love action.
3.       Who allows him to be her protector now and then.
4.       Who will make sure he does not get lost in the crowd.
5.       To be his strength when he is weak.
6.       Who understands that boys like big toys.
7.       To teach him that he can be competitive without being ruthless.
8.       To teach him to avoid selfish temptation.
9.       To teach him to try harder when given a second chance.
10.   To teach him that family is more important than work.
11.   To tell him that jealousy can ruin relationship.
12.   Who knows how to have fun.
13.   To teach him the art of listening.
14.   Who knows where to find what he has misplaced.
15.   Who understands that what he needs from her changes as he grows older.
16.   Who leads him towards his talents and passions.
17.   Who is never more than a phone call away.
18.   To make sure he finishes his home work first.
19.    Who is always excited to hear his news.
20.   To teach him that a sense of humor will never lose its luster.
21.   To let him know it is okay to cry.
22.   To be his first dance partner.
23.   To show him what it means to love unconditionally.
24.   To help him to the details girls will notice.
25.   Who is always there for him, even if by mail.
26.   Who will let him go when he is ready to marry.
27.    To help prepare him for being a father.
28.   To fill his childhood with love and affection.
29.   Who will always make sure he has a home to come back to.
30.   Who shows him that men and women are equals.
31.   Whose arms, heart and mind are always open.
32.   Who will not fail to discipline him for his misdeeds.
33.   Who never tires of his hugs and kisses.
34.   To help him understand and respect personal space.
35.   To teach him how to conduct himself like a gentleman.
36.   To advise him when he falls in love.
37.   To teach him to be a force of kindness in the world.
38.   To explain to him what he cannot yet understand.
39.   To tell him that there is more to being a man than being tough.
40.   To teach him how to show love without restraint.
41.   Because without her he will have less in his life than he deserves.
42.   To tell him he is handsome.
43.   To teach him to play fair.
44.   To help him see the richness of diversity.
45.   To teach him that embarrassment is not a reason for quitting. 
46.   To believe in him even when it seems no one else does.
47.   To be his trusted confidante.
48.    To make sure he looks his best before leaving the house.
49.   To encourage him to be serious.
50.   To make sacrifices so he will not have to sacrifice.
51.   To teach him the importance of compromise.
52.   To steer him away from darkness.
53.   To protect him until he is old enough to protect himself.
54.   To tell him that women admire a sincere apology.
55.   To teach him that he should be humble.
56.   To teach him table manners.
57.   To teach him that he should be humble.
58.   To teach him to show appreciation for what others have done for him.
59.   To teach him that all people are worthy of respect.
60.   To help him overcome his fears.
61.   To make sure his socks match.
62.   Who doesn’t forget that boys will be boys.
63.   To tell him often that he is loved.
64.   To hold him when he needs comfort.
65.   To help him understand that things will not always go his way.
66.   To teach him to pay attention to the small things.
67.   To teach him the pitfalls of hypocrisy.
68.   To teach him that every fight isn’t worth fighting.
69.   Who understands the pleasure of a good pillow fight.
70.   Who will let him be himself.
71.   To remind him to say his prayers.
72.   To make sure his world has a broad horizon.
73.   Who sees the humor in his silly ways.
74.   Who insists that he do his fair share of the household chores.
75.   Who will stand up to him when he is wrong.
76.   Who encourages self- expression.
77.   To make sure he has good memories to hold on to.
78.   To make sure he begins his day on the right foot.
79.   To teach him how to take care of himself.
80.   To teach him that sometimes the battle is within.
81.   To make sure that faith is the light that guides him.
82.   To tell him that anything is possible if done for the right reason.
83.   To tell him that remaining faithful is his promise and obligation.
84.   Who does not hold him back when he is ready to take the next step.
85.   Who is there for him no matter what is age.
86.   To make his favorite food on his birthday.
87.   To help him learn how to laugh at himself.
88.   To help him develop the habits girls prize.
89.   To teach him that being subtle can be narrative.
90.   To teach him how to flirt without making a fool of himself.
91.   To tell him about the miracle of life.
92.   To show him to take one day at a time.
93.   To make sure he attends to his mind, as well as his body.
94.   To insist that he be respectful of women.
95.   To teach him that admitting ones mistake is a sign of strength, not weakness.
96.    To tell him that he cannot change others, but he can learn to accept them for whom they are.
97.   To make sure he does not get lost.
98.   Who will always be there to wipe his tears.
99.   Who will show him the right way to path.
100.who will be there to accept his apology.